Mfanyakazi wa sulubu kwenye duka moja kuu jijini auawa na lifti mbovu kazini
23rd October, 2014
Mtu mmoja amefariki papo hapo baada ya lifti aliyokuwemo ndani akipakia mizigo katika duka la Tuskys Nairobi kuanguka kutoka gorofa ya nne eneo la chini la jumba hilo maarufu kama basement. Kisa hicho kimeibua ukosoaji mkubwa huku waliokuwamo dukani wakilalamikia ukuu- kuu wa mashine zinazotumiwa na wafanyakazi kwenye baadhi ya maduka makuu jijini. Lofty Matambo na taarifa hiyo.