Serikali ya Kenya yalaumiwa kwa kushindwa kuwatetea raia wake wanaofanya kazi Mashariki ya Kati
22nd October, 2014
Serikali ya Kenya imelaumiwa pakubwa kwa kushindwa kuwatetea raia wake wanaofanya kazi za ujakazi Mashariki ya Kati. Siku chache baada ya Wizara ya Leba kupiga marufuku mawakala wote wanaowapa Wakenya ajira Ughaibuni, Wakenya ambao sasa wanahudumu hasa nchini Saudi Arabia wameendelea kupitia mahangaiko bila kuona mkono wa ubalozi wa Kenya. Saida Swaleh