Gavana Ukur Yatani akosoa Magavana kwa kushinikiza kufanyika kwa Kura ya Maamuzi
16th September, 2014
Gavana wa Marsabit Ukur Yatani amewakosoa Magavana wenzake kwa kushinikiza kufanyika kwa Kura ya Maamuzi . Yatani amesema kuwa ni vyema kwa magavana kufanya mazungumzo na serikali ndiposa waongezewe fedha za kaunti badala ya kupoteza muda mwingi katika kuwashwaishi wakenya kuunga mkono kura ya maamuzi. Yatani ameyasema haya alipozuru afisi a shirika la standfard group ambapo pia alieleza hamu ya serikali yake kuungana na shirika hili katika kuhamasisha ustawi na maendeleo katika Kaunti ya Marsabit.