Polisi watumia vitoa machozi kuwatawanya waliokwa wakizua rapsha katika Barabara Kuu ya Thika
9th September, 2014
Maafisa wa polisi katika Barabara Kuu ya Thika, eneo la Githurai walilazimika kutumia vitoa machozi kuwatawanya wananchi waliofunga barabara hiyo wakilalamikia hukumu iliyotolewa kwa askari mmoja kwa mauaji ya watu wawili katika eneo hilo. Ni tukio lililowastaajabisha wengi, kwani aliyekuwa akitetetewa na raia kwa wakati huu alikuwa ni afisa wa polisi.