Shule ya State House Girls wapokea basi mpya kutoka kwa Rais Uhuru Kenyatta
25th July, 2014
Rais Uhuru Kenyatta hii leo aliwafurahisha wanafunzi wa shule ya upili ya statehouse girls kwa kuwanunulia basi la shule . rais kenyatta ambaye aliwasili kwenye shule hiyo akiwa ndani ya basi hilo alilakiwa na wanafunzi hao kwa furaha kuu.
Baada ya kushuka rais alisindikizwa na gwaride la wanaskauti wa shule hiyo hadi kwenye sherehe ya kuwapa hidaya hiyo wanafunzi hao akishirikiana na mkewe margret kenyatta mapema katika sherehe hiyo wanafunzi hao wa kike walikuwa wamekariri shairi la kumsihi mkewe rais kuwasaidia kununua basi jipya kwani lile walilokuwa wakitumia limechakaa. rais kenyatta alikuwa amewaahidi wanafunzi hao basi mara ya mwisho alipowatembelea.