Mbunge wa Nyando Fred Outa afadhi kiti chake katika mahamuzi ya Mahakama ya Juu
3rd July, 2014
Mbunge wa eneo bunge la Nyando, kaunti ya Kisumu Fred Outa leo amepata afueni baada ya mahakama ya juu kutupilia mbali kesi dhidi ya uchaguzi wake.
kesi hiyo ambayo iliwasilishwa na jared okello ilifutiliwa mbali na majaji wa mahakama ya juu kalpana rawal, smokin wanjala, njoki ndung’u, jackton ojwang’ na mohammed ibrahim. mwezi wa machi mwaka huu, mahakama ya rufaa ilitoa uamuzi kwamba fred outa hakuchaguliwa kwa njia halali baada ya madai ya kuwahonga wapiga kura kwa kutumia pesa za cdf. outa alifika katika mahakama ya juu akipinga uamuzi huo huku akisema hii leo ameridhishwa na uamuzi huo alioutaja kuwa wa haki