Baadhi ya matatu mjini zawekwa mtandao wa Wifi
14th June, 2013
Muziki ndani ya matatu ulipoanza, ikawa maendeleo, video kama umetulia ndani zikafuatia na sasa abiria wataenjoy huduma za mtandao wa internet maarufu kama wifi bure bilashi. Kampuni ya mawasiliano ya safaricom imezindua mpango na wa kwanza kufaidika ilikuwa matatu za kuelekea buruburu. Rongai na kayole tayari abiria wao walikuwa wameanza kufaidi mtandao ndani ya matatu. Swali kuu hata hivyo je pande zote husika zimetafakari swala la usalama hasa abiria kuporwa simu?