Benki ya Co-operative
9th August, 2012
Benki ya Co-operative imenakili ongezeko la asilimia 21.7 ya faida zake katika kipindi cha miezi sita iliyokamilika kabla ya kutozwa ushuru. Kulingana na afisa mkuu wa benki hii Gideon Muriuki, benki hiyo imenakili faida ya shilingi bilioni 4 ikilinganishwa na shilingi bilioni 3.3 ilizopata katika kipindi sawa na hicho mwaka jana. Kiwango cha mikopo ilichotoa katika kipindi hicho vile vile kimeongezeka kwa asilimia 18.3. Katika kipindi hicho benki hiyo imetoa mikopo ya jumla ya shilingi bilioni 112.6. Meneja mkurugenzi wa benki hiyo Gideon Muriuki amesema ongezeko la viwango vya riba katika benki kuu iliathiri utoaji wa mikopo kwa wateja wa benki hiyo katika kipindi hicho.