Darubini 1.
Wawanie urais-Wamalwa
Siku chache tu baada ya mahakama ya ICC kutangaza siku ambazo kesi dhidi ya Wakenya wanne zitaanza, Waziri wa Haki na Masuala ya Katiba Eugene Wamalwa amesema kuwa Naibu Waziri Mkuu Uhuru Kenyatta na Mbunge wa Eldoret Kaskazini William Ruto wako huru kuwania urais kwenye uchaguzi mkuu ujao. Suala hilo ndilo tunaloliangazia kwenye darubini yatu. Kugombea kwa Uhuru na Ruto kutaathiri vipi uchaguzi? Je, kuwania huko kutawezesha duru ya pili ya uchaguzi kuwapo ama vigogo hao watapata uungwaji mkono na kumpiku Raila Odinga kwenye duru ya kwanza? Beatrice Maganga anafungua darubini hii.
Posted on July 12, 2012 na Beatrice Maganga
